Thursday, March 22, 2012

FAINALI ZA SAFARI LAGER NYAMA CHOMA

Fainali za Safari Lager Nyama Choma jijini Mwanza yafana sana ndani ya viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.

Mgeni Rasmi katika Fainali za Mashindano ya Safari Lager Nyama Choma,Bw. Said Mbweche kutoka (mwenye suti nyeusi) akizungumza machache kabla ya kuanza kutoa zawadi wa washindi mbali mbali wa Mashindano hayo yaliyofanyika leo na kufana sana kwenye viwanja vya Furahisha Mwanza.Wengine Pichani ni wakuu wa idara ya Masoko ya TBL,Majaji wa Mashindano hayo (mwenye mavazi meupe) pamoja na Wadau wa Safari Lager.

Nyama ikiwa jikoni

Nyama ikiandaliwa tayari kwa kwenda kwa wateja waliohudhulia fainali hizo za Safari Lager Nyama Choma.
Nyama ikiendele kuiva jikoni.
Muwakilishi wa Bar ya Shoken ambao ndio Washindi wa Kwanza wa Mashindano ya Safari Lager Nyama Choma jijini Mwanza ,Bw. Kavishe akipokea zawadi yake ya fedha taslim kiasi cha sh. Mil. 1 kutoka kwa Mgeni Rasmi,Bw. Said Mbweche.
Muwakilishi wa  AR Bar ambao ni washindi wa Pili akifurahia nafasi aliyoipata.
Muwakilishi wa Victoria prince Bar.
Muwakilishi wa Villa park Bar akichukua zawadi yake ya kushika nafasi ya tano.
Mgeni Rasmi katika Fainali za Mashindano ya Safari Lager Nyama Choma,Bw. Said Mbweche (mwenye suti nyeusi) akizungumza machache kabla ya kuanza kutoa zawadi wa washindi mbali mbali wa Mashindano hayo yaliyofanyika leo na kufana sana kwenye viwanja vya Furahisha Mwanza,Katikati ni Meneja wa Bia ya Safari Lager,Oscer Shelukindo na Kushoto ni Meneja Mauzo wa TBL,Flavian Ngole.
Furaha ya Ushindi kwa Wadau wa Shokeni Bar.
Wadau wa TBL.
Wadau mbalimbali wakiangalia mashindano yanavyoendelea.
Wadau mbalimbali wakiangalia mashindano yanavyoendelea.

Prepared by:  Elicy Michael.

Monday, March 19, 2012

UMOJA WA MICHEZO VYUONI.

Michezo huleta mahusiano mazuri miongoni mwa jamii husika.Uwepo wa mashindano yatakayohusisha vyuo vikuu mbalimbali vya nchini Tanzania na hata nchi za jirani utasaidia kujenga umoja miongoni mwa vyuo husika.(Richard Kidubo.)

Saturday, March 17, 2012

KIGALI TUNAENDA.

Baadhi ya wana Group 19 wakiwa wanatoka  Kirumba kuangalia mechi kati ya BAPRM3  na Toto African sport club japo BAPRM 3 walifungwa  lakini walionesha  soka safi.(Maheta   Abdu)

USIBWETEKE KAKA.

Moja ya  wachezaji anaeongoza  katika  Ufungaji  wa timu  ya  PR3 Emmanuel  Lyogohya  akiwasikiliza wanagroup wake.(Mwijukia   Martha)

HONGERA SAANAAAAAAAAAAAAAA.

 Meneja msaidizi  wa timu ya PR 3 akimpa hongera  mfungaji  wa magoli  mawili zidi  ya timu ya sheria mwaka wa nne LLB 4  ndugu  Emmanuel lyogohya ambapo timu ya PR ilishinda   3-1.(By   Abdul   Afsa)

HAIWEZEKANI TWENDENI.

Baadhi ya kina dada kutoka BAPRM 3 wakiwa wanaelekea uwanja wa kirumba kuangalia mechi ya majaribio kati ya PR 3 na timu inayoshiriki Ligi kuu ya Tanzania Toto African ya mwanza ambapo timu ya Toto African iliibuka na Ushindi wa goli 8-1.(By  Emmanuel  lyogohya)

MENEJA KAZINI.

Meneja msaidizi wa timu ya Mahusiano ya Umma na Masoko ABDU   RASOUL (BAPRM 3) akibadilishana mawazo na wadau kwajili ya kuisaidia timu katika mashindano ya FAWASCO (By  Nyanzala   Constatine)

MAHUSIANO KWA UMMA NA MICHEZO.

Hii ni blog ambayo itakuletea mambo mbalimbali ya michezo na burudani,hivyo kaa tayari kupata mengi kutoka blog hii iliyosheheni wataalamu katika tasnia hii ya mahusiano na masoko.Karibuni sana!