Wachezaji wa Simba wakiwa wamembeba Kocha wao, Milovan Cirkovic,
baada ya kuifunga Moro United 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka
Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
salaam. Kwa ushindi huu Simba imejitangazia ubingwa. Kinachosubiriwa ni
mchezo wao wa kufunga ligi na Yanga.
Simba wakifurahia ushindi
Mashabiki wakiruka kidedea
Kiduku kilitawala ushindi huo ambapo Wekundu hawa wa Msimbazi wamejitangazia ubingwa huku wakisubiri mchezo wao wa mwisho wa ligi na Yanga.(Habari na ELICY MICHAEL)
No comments:
Post a Comment