Wednesday, May 23, 2012

HII NDIO GARI ILIYOCHUKUA UHAI WA KIPENZI CHETU MAFISANGO - WENZAKE WANNE WANASURIKA

HII NDIO GARI ILIYOCHUKUA UHAI WA KIPENZI CHETU MAFISANGO - WENZAKE WANNE WANASURIKA:


Ndugu yake Mafisango aliekua nae wakati wa ajali amesema Mafisango alifariki dunia hapohapo kwenye ajali wakati wakitoka Club kuelekea nyumbani, walipofika kwenye taa za barabarani Tazara Dar es salaam, Mafisango ambae ndio alikua anaendesha alijaribu kuziwahi taa lakini ghafla akakutana na mwendesha guta ambapo katika kumkwepa gari ilimshinda na kuingia mtaroni leo Alfajiri.

Alikua na wenzake watano kwenye gari ambapo wengine wanne wamepona japoa walipata majeraha madogo madogo akiwemo mdogo wake ambae amesajiliwa na club ya Simba.

Haruna Niyonzima mchezaji wa Yanga alikua mchezaji wa mwisho kubadilishana jezi na Mafisango Tanzania, katika mechi ambayo Mafisango alifunga goli lake la mwisho.

Anasema Ijumaa ndio Mafisango alimwambia atasafiri kwenda Rwanda kujiunga na kikosi cha timu ya taifa, hili ni pigo kwa Tanzania, Rwanda na hata Congo DRC.

Na Elicy Michael

No comments:

Post a Comment