Wednesday, May 2, 2012

KOCHA MPYA WA ENGLAND

KOCHA MPYA WA ENGLAND: NITAONGEA NA RIO NA TERRY, ROONEY ATAKUWEMO KATIKA KIKOSI CHANGU - SHEARER ATAJWA KUWA MSAIDIZI WAKE

 

 Kocha mpya wa England Roy Hodgson ataongea na John Terry na Rio Ferdinand kwa matumaini ya kuwachukua wachezaji wote wawili katika michuano ya EURO 2012.

Kazi kubwa ya kwanza kwa Hodgson ni kunitibu majeraha ya uhusiano mbovu uliopo baina ya wachezaji  katika chumba cha kubadilishia nguo uliotokea baada ya Terry kutuhumiwa kumtolea maneno ya kibaguzi Antoni Ferdinand - ambaye ni mdogo wake Rio. mwezi October mwaka jana.

Terry na Ferdinand wanabakia kuwa mabeki wenye ushirikiano mzuri katika timu ya taifa na wakati akitangazwa rasmi katika uwanja wa Wembley, Roy alikaririwa akisema: "Itabidi niongee na John na Rio, natumaini tutakutana uso kwa uso, na kujua nini suluhisho.

"Kwa sasa siwezi kusema chochote  mpaka nitakapogundua kiundani mahusiano yao yapoje - na nafikiri sitoongeea na wao tu, nitaongea na wachezaji wote wakubwa ndani ya kikosi."

Hodgson, ambaye amesema kwamba atamchagua Wayne Rooney katika kikosi cha wachezaji 23 - ambacho atakitangaza muda mfupi baada ya msimu kuisha - bado hajaamua kuhusu wasaidizi wake.

Lakini inaaminika atamchagua msaidizi mmoja, ingawa bado hajaongea na kocha wa England chini ya miaka 21 na kocha wa timu ya Uingereza ya Olympic Staurt Pearce kuhusu jinsi ya kuhusika kwake katika EURO 2012.

 

Mtu anayetajwa sana kuweza kuchaguliwa kama msaidizi wa Roy ni Alan Shearer ambaye anatajwa kuwa na mahusiano ya karibu sana na Hodgson.(Na Elicy Michael)

 

No comments:

Post a Comment