Kikosi cha timu ya Taifa ya Lesotho.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akisalimiana na wachezaji wa timu ya
Taifa ya Netiboli ya Tanzania 'Taifa Queens'wakati ufunguzi wa
mashindano ya Afrika yaliyoanza leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam, ambapo Tanzania imeichapa Lesotho kwa 57-13
Wanamuziki wa Bendi ya Mwenge Jazz wakitumbuiza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Afrika ya Netiboli.
Mlinzi wa timu ya taifa ya Netiboli Tanzania, ‘Taifa Queens’, Lilian
Sylidion (kushoto), akiwania mpira mbele ya wachezaji wa timu ya Lesotho
katika mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Afrika uliofanyika leo
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Taifa Queen's imeshinda
57-13.
Kikosi cha Taifa Queen's. Na Elicy Michael
No comments:
Post a Comment